Ni Estomi Elieza, Mfanyakazi Hodari wa BUWSSA kwa mwaka 2025

Mnamo tarehe 23 Aprili 2025, Mkutano Mkuu wa Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWSSA) umefanyika na kumchagua Bwana Estomi Elieza, Mtumishi kutoka Idara ya Usambazaji Maji na Usimamizi wa Usafi, kuwa Mfanyakazi Hodari wa BUWSSA kwa mwaka 2025.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Meneja Rasilimaliwatu na Utawala wa BUWSSA, Bwana Abdulrahmani Kombo, amesema kuwa Bwana Estomi ameibuka kidedea baada ya kupata kura 21 kati ya kura 34 zilizopigwa. Bwana Kombo amewapongeza na kuwashukuru watumishi wote kwa kushiriki uchaguzi huo kwa haki, uwazi na kuzingatia vigezo vilivyowekwa.

Kwa upande wake, Mfanyakazi Hodari wa mwaka 2025, Bwana Estomi Elieza, amewashukuru watumishi wote kwa kumuamini na kuridhishwa na utendaji wake. Pia ameahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, nidhamu na ushirikiano mkubwa kwa manufaa ya Mamlaka na wananchi wanaohudumiwa na BUWSSA.

BUWSSA, Kazi Iendelee.!!!

Be the first to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published.


*