BODI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira  Bunda (BUWSSA) inaendeshwa na Bodi ya Wakurugenzi wapatao 8 ambao huteuliwa kuwakilisha vikundi au makundi ya watu katika jamii ya watumiaji maji wa Mji wa Bunda kulingana na umuhimu wa kila kundi.

1.  MUUNDO WA BODI YA WAKURUGENZI

  1. Mwenyekiti wa bodi.
  2. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji.
  3. Mkurugenzi Mtendaji wa BUWSSA
  4. Mwakilishi wa Madiwani.
  5. Mwakilishi wa kundi la Watumiaji wakubwa.
  6. Mwakilishi wa kundi la Wafanya Biashara.
  7. Mwakilishi wa kundi la Watumiaji maji Majumbani.
  8. Mwakilishi kutoka Wizara ya Maji.

2.  MAJUKUMU MAKUU YA BODI

  • Kusimamia na kutathimini shughuli zote za Mamlaka.
  • Kupitisha mipango ya kazi na Bajeti.
  • Kiungo kati ya Wizara na Mamlaka.
  • Kuajiri na kuachisha kazi watumishi.
  • Kuwawakilisha wateja na kusikiliza malalamiko yao pamoja na wadau.
  • Kusikiliza maoni ya watumishi na kutoa ushauri.