JINSI YA KUFANYA MALIPO

MAELEZO YA JINSI YA KULIPIA BILL (MAELEZO KWA MTEJA)

  1. KWA NJIA YA SIMU ZA KIGANJANI
  • Malipo yanaweza kufanyika kupitia huduma za simu za kiganjani (TIGOPESA, M-PESA, AIRTELMONEY, T-PESA, HALOPESA, EZYPESA) kwa kupitia mitandao mbalimbali ya simu kama ifuatavyo;
  • Ingia kwenye menu ya mtandao husika
  • Chagua 4 (Lipa Bili)
  • Chagua 5 (Malipo ya Serikali)
  • Ingiza Namba ya kumbukumbu ya malipo (Iliyopo kwenye bili)
  • Ingiza kiasi cha pesa
  • Weka namba ya siri

 

Namna ya kulipia kwa Tigopesa

  1. Piga *150*01#
  2. Chagua namba (4) “Lipa Bili”
  3. Chagua (5) “Malipo ya Serikali”
  4. Ingiza namba ya kumbukumbu ya malipo (Control number)
  5. Ingiza kiasi cha pesa unachotaka kulipa
  6. Ingiza namba ya siri kuhakiki

Namna ya kulipia kwa M-Pesa

  1. Piga *150*00#
  2. Chagua namba (4) “Lipa kwa M-Pesa”
  3. Chagua (5) “Malipo ya Serikali”
  4. Chagua namba 1 Namba ya Malipo
  5. Ingiza namba ya kumbukumbu ya malipo (Control Number)
  6. Ingiza kiasi cha pesa unachotaka kulipa
  7. Ingiza namba ya siri
  8. Thibitisha kwa kuchagua (1)

 

Namna ya kulipia kwa airtelmoney

  1. Piga *150*60#
  2. Chagua namba (5) “Lipia Bili”
  3. Chagua (5) “Malipo ya Serikali”
  4. Chagua namba 1 “Weka namba ya kumbukumbu”
  5. Ingiza namba ya kumbukumbu ya malipo (control number)
  6. Ingiza kiasi cha pesa
  7. Weka namba ya siri

 

Namna ya kulipia kwa T-Pesa

  1. Piga *150*71#
  2. Chagua namba (5) “Lipia Bili”
  3. Chagua (3) “Malipo ya Serikali”
  4. Ingiza kumbukumbu namba (control number)
  5. Ingiza kiasi
  6. Ingiza namba ya siri

 

Namna ya kulipia kwa halopesa

  1. Piga *150*88#
  2. Chagua namba (5) lipia bili
  3. Chagua (5) malipo ya serikali
  4. Weka namba ya kumbukumbu ya malipo (control number)
  5. Ingiza kiasi cha pesa
  6. Weka namba ya siri

 

Namna ya kulipia kwa Ezypesa

  1. Piga *150*02#
  2. Chagua namba (8) malipo ya serikali
  3. Chagua (1) Tanzania Bara
  4. Weka namba ya kumbukumbu ya malipo (control number)
  5. Ingiza kiasi cha pesa
  6. Weka namba ya siri
  1. KWA NJIA YA KUWEKA FEDHA BENKI (DIRECT BANK DEPOSIT)

Malipo yanaweza kufanyika kwa kuweka fedha katika benki zifuatazo, mfano: NMB, CRDB kwa kupitia matawi ya benki, mawakala wa Benki na njia nyingine za malipo zitolewazo na Benki. Tumia Namba ya kumbukumbu ya Malipo (Control Number) uliyopewa unapofanya Malipo.

 

  1. KWA NJIA YA KUHAMISHA FEDHA (TISS)

Malipo yanaweza kufanyika kwa njia ya kuhamisha Fedha kutoka benki moja kwenda benki nyingine ndani ya Tanzania (TISS). Mteja / Mlipaji atapatiwa fomu za kuhamishia fedha na Mamlaka ya Maji Bunda baada ya kuichapisha (Printed Transfer Form / Bill) na ataipeleka na kuiwasilisha katika benki atakayoitumia kuhamisha fedha na hatatakiwa kujaza upya fomu.