USITISHAJI NA UREJESHAJI WA HUDUMA YA MAJI KWA MTEJA

KUSITISHIWA HUDUMA YA MAJI KWA MTEJA

  1. Mamlaka itamuondolea huduma mteja atakayeshindwa kulipa ankara ya mwezi baada ya siku 30 tangu alipopata Ankara ya maji.
  2. Wateja wanaweza wasipewe taarifa nyingine ya ziada zaidi ya iliyoko kwenye Ankara ya madai ambayo ni notisi iliyojitosheleza kabla ya kusitishiwa huduma.
  3. Kusitishwa kwa huduma kutafanyika wakati wowote endapo mteja atagundulika kuwa anatumia maji kinyume na sheria na kwa njia isivyo halali. Hatua hii itaenda sambamba na kuchukuliwa hatua za kisheria.
  4. Wateja waliowahi kuondolewa kwenye huduma na kukutwa wamejirudishia huduma isivyo halali wataondolewa tena kwenye huduma na kuchukuliwa hatua za kisheria.
  5. Mamlaka haitamuondolea mteja huduma siku zifuatazo;

UREJESHWAJI WA HUDUMA

  1. Mteja atakayesitishiwa huduma ya maji kwa kutolipia ankara atarejeshewa huduma baada ya kulipa deni analodaiwa na adhabu ya kutolipa deni husika kwa wakati ndani ya masaa 24.
  2. Wateja watakao ondolewa huduma kutokana na kujiunganishia huduma ya maji bila halali watarejeshewa huduma baada ya kulipa ada husika, fidia ya maji waliyotumia na adhabu.
  3. Baada ya kukubaliana na Mamlaka kuhusu namna ya kulipa deni.
  4. Baada ya kubaini kwa uhakika kwamba mteja aliondolewa huduma kimakosa.
  5. Kama uondoaji huo ulitokana na shughuli za kiutendaji na kiufundi za Mamlaka.